Psalms 129

Maombi Dhidi Ya Adui Za Israeli

Wimbo wa kwenda juu.

1 aWamenionea mno tangu ujana wangu;
Israeli na aseme sasa:
2 bwamenionea mno tangu ujana wangu,
lakini bado hawajanishinda.
3 cWakulima wamelima mgongo wangu,
na kufanya mifereji yao mirefu.
4 dLakini Bwana ni mwenye haki;
amenifungua toka kamba za waovu.

5 eWale wote waichukiao Sayuni
na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 fWawe kama majani juu ya paa,
ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 gkwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,
wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 hWale wapitao karibu na wasiseme,
“Baraka ya Bwana iwe juu yako;
tunakubariki katika jina la Bwana.”
Copyright information for SwhNEN